Mahusiano nyota ya Nge na Kaa (Scorpio and Cancer)

Rakims

 Nge na Kaa

Utangamano

(Scorpio and Cancer)









Nge & Kaa Chumbani na urafiki wa karibu Utangamano wenu:

Nyota yako kwanza kabisa inahusiana na kifo na kila aina ya jambo baya kwa maana ina tawala mlango wa nane (House of dealth and regeneration). na vile vile wenye nyota yako sifa hizi mbaya huja kutokana na hisia kali ulizonazo na pia ukandamizaji wako katika tendo la ndoa,
Kwenye mahusiano yeye (Kaa) mara nyingi ni mwenye kukuelewa zaidi hasa linapokuja suala la kuelezia hisia zako nzito kwake na kwa mambo mengine pia. Unatarajiwa kuwa na giza kubwa sana la wimbi la ngono hata kama utakuta unajizuia vipi. Na hii hupelekewa pale yeye atakaposhindwa au kuogopa kuhimili mikiki mikiki yako ya chumbani, vile vile mahusiano yenu kingono ni mazito sana na matamu kuliko kawaida unless uwe na matatizo ya kisaikolojia ila kama kati yenu hakuna mtu mwenye matatizo basi mahusiano kati ya Nge na kaa ni mahusiano ambayo watu wengi wanatamani kuwa nayo kwa maana ukiskia moja kati ya real love ndio hii couple. 

Mahusiano haya ya nyota hizi mbili za asili ya maji yaani maji ya moto na maji ya bahari ni yenye kuvutia na kupendeza machoni kwa watu kwa jinsi mnavyokuwa hata mbele za watu. Kwa hapa hujakosea kama hujafunga ndoa basi nenda hata kafunge kesho.

Hii ni zawadi kubwa kuwa na mahusiano haya. Yeye(Kaa) ni mpenzi hasi na wewe (Nge) ni mpenzi chanya na vile vile kuna moto mkali wa mahaba unaotoka kwako kwenda kwake katika wimbi la kiroho ambao unapelekea mahusiano haya kuwa madhubuti. Joto la chumbani pia ni habari nyingine hapa mnafaana na kuendana sana.
Joto hilo la chumbani huamsha hisia kali na hupelekea kichochezi cha wawili nyie kuoneana wivu wa kupindukia.
Wewe ni mwenye kumjanza nguvu na ulinzi wa hali ya juu na yeye ndicho kitu ambacho anatafuta zaidi kwenye mahusiano kwa maneno mengine anaweza kukuita soul mate. Yeye ni mwenye kwenda sawa na kila mtu ni mtu wa watu na mwenye kupenda watu wote sio mbaguzi na anapokuwa na wewe hili huwa dhahiri kwake, na ni kitu ambacho wewe unapenda kukiona kiwepo kwa mwenza wako. Nyie wawili mnaendana kama mkate na Jam.

Haya ni mahusiano kati ya nyota mbili za maji ambapo mapenzi yenu kila mmoja anataka na kupendezewa kuona hisia kali kwa mwengine na ni kitu ambacho wote wawili kila mmoja yupo radhi kumgawia mwenzie bila choyo wala kumbania, Mnapoingia kwenye mahusiano basi mnakuwa na upendo usio na mipaka na urafiki wakaribu kwenu hushamiri na watu wengine hapa inategemea wa kike ni nani na wa kiume ni nani kwa maana kuna mmoja akiwa jinsia fulani basi mnaweza kuwa kama mtu na shoga yake yaani urafiki wenu hukithiri hadi kuanza matani ya kuonana mtu na shoga yake walioshibana.

Ingawa sasa nyota yako ya Nge ni nyota ya mtu ambaye ni sawa na mbalamwezi iliyodondoka ambayo mbalamwezi ni sayari ya nyota ya kaa kinajimu kwake wewe ni sawa na baba au mama kutegemea na jinsia yako. Sasa kama wewe hisia zako zikichanganyika na ukali basi mahusiano yenu yatakuwa ni sawa na mapenzi ya ugomvi wenye hisia za mahaba makali ndani yake yaani mnaweza kutukanana kisha mkacheka Isipokuwa baadae hii itakuja kumchosha yeye na vile uombaji wako wa tendo mara zingine umetawala mabavu na shari.

Kwa hivyo hapa mtakuwa mnaendana kwa asilimia 90%

Nge & Kaa uaminifu wenu

Wewe (Nge) unapopenda moja kati ya jambo kubwa kwenye mahusiano yako huwa ni Uaminifu, Ikifikia sehemu umejihisi kusalitiwa basi mara nyingi huonyesha wivu wako wote na uchungu sana bila kuficha na kila mtu aliyekaribu yako atajua kuwa umesalitiwa.
Lakini sasa kwa mwenza huyu (Kaa) anapoingia kwenye mapenzi yeye hupenda kuheshimu sana mpenzi wake na kumlindia kwa hali zote kumuhifadhia utu wake kwa maana moja kwa moja ni rahisi sana kwake yeye kujua kuwa hapa akicheza kitim tim chako ni kivumbi cha hatari kwenye wivu.

Na nyote vile ni wenye asili ya maji mara nyingi ni watu ambao usaliti kwenu kila mmoja ni kitu anachopenda kufanya japo ni wenye mapenzi ya dhati kila mmoja kwa mwenzie hivyo kwa ugumu kidogo mwanzo kwenye uaminifu mapenzi yatayumba lakini baada uaminifu huja kwa upana sana kwa maana kila mmoja kati yenu anajua ni jinsi gani mapenzi yanauma.
Moja kwa moja nyote wawili ni wenye kupeana ulinzi wa mahaba na wote mtajihisi kuhifadhika hapo baadae.

Hivyo linapokuja suala la uaminifu mnaendana kwa asilimia 95%

Nge na Kaa mawasiliano yenu na mazungumzo:
Wawili nyie ni wenye kuelewana hata kama pasipohitajika mazungumzo yaani sura tu huonyesha kujielezea kwa kila mmoja wenu. Hii pia huweza kuinfluence maisha yenu ya tendo la ndoa na kulifanya kuwa bora kuliko watu wengine. Lakini vile vile hii inaweza kuwa ni yeye kuleta mtafaruku kama mapenzi ya mwingine yataelemea katika kitu fulani tuchukulie mfano hajakupenda wewe na kapenda kile ulichonacho. Mazungumzo yenu ni mazuri sana kwa kuwa tu mara nyingi huhusisha hisia zenu. Na hata muda mwingine kwa wale wanaoanza urafiki utaona ni wepesi kila mmoja kumalizia sentensi ya mwenzie. Wote ni wenye kupenda kuzungumza mara kwa mara ingawa hili mwanzoni sio rahisi kuonekana na mara nyingi kwako wewe ni mwenye kupenda kujiweka hupendi maneno na una katabia ka kuexaggerate mambo.

Ikitokea yeye akaanza kukuona tofauti mwanzo basi moja kwa moja atashindwa hapo hapo mwanzoni kuendelea na wewe na atatafuta kila njia ili kila mtu ashike nafasi yake. Lakini hii ni ngumu kwa maana mkiwa pamoja kila mmoja wenu anatamani na kutaka kuhakikisha anamuweka mwenzie sawa vile anavyopenda aende nae yeye.

Hivyo tunapokuja kwenye maelewano yenu mnaendana kwa asilimia 99%

Nge na kaa Hisia zenu:

Hii ni nyeti sana na tawala ya kimbinu sana kwenye mahusiano kama haya.
Yeye ni mwenye kupenda sana kuishia na hisia zake au kuzificha ikiwa ni zenye faida au hasara yeye hupenda kuficha sana hisia zake.Na pia hupenda zaidi na pia katika kutumia hisia zake katika maisha yake ya kila siku basi utakuta moja kwa moja yeye ni mwenye kukuletea ugumu kuelewa kwenda na hisia zake, kwa sababu ana uwezo mkubwa wa kupotezea na kuficha hisia zake.
na akili taka lake kihisia hashindwi kupata na ni mtu rahisi sana kucheza na hisia za mtu anaweza akakujaza kisha akakuacha kwenye mataa. Kitu kinachowasaidia kwenye mahusiano yenu ni ile hali ya kila mtu kuwa na uwezo wa kustahamili mwenzie na hisia ni vitu vinavyohitajika ili mahusiano yakue japo hazina nafasi sana ya kuingilia mafanikio ya uhusiano wenu kwa maana ni kitu wewe huwa unajiamini kuwa ni cha kupanda na kushuka.
Nyote wawili mnatakiwa kujifunza jinsi ya kuachia ngazi kwenye mahusiano ya utawala isiwe mmoja ni mwenye kung;ang'ania mahusiano ya utawala ulalie kwake tu. Hii itasaidia sana katika kukuza mahusiano yenu.

Kwa hali hii kwenye suala la hisia mnaendana kwa asilimia 70%

Nge na Kaa Thamani:

Linapokuja katika suala la kuthaminiana hapa huwa kuna mtiti kwa maana yeye ni mbinafsi katika suala la thamani na ni mwenye kutaka familia yenye kumtegemea yeye tu. kwenye familia huyu ni mbinafsi na bahili, Lakini kwenye familia wewe ni mtu wa kujiachia na inapokuja kwenye kuthaminiana wewe huthamini mwanzo wa thamani yenyewe kisha baadae kushusha kisha kupanda yani wewe kwake suala la thamani ni jambo la kupanda na kushuka. Ni ngumu na ugumu kwenu huja kwenye suala la kuthaminiana hata mjitahidi vipi ugomvi wenu mkubwa utakuwa ni kuchanganya maana ya neno thamani na kujali.
Mahusiano haya yana ubovu katika matumizi ya neno hunijali na hunithamini sawa na kulinganisha pumba na mchele time zote pumba utaona mchele na mchele utaona pumba na kusahau kuwa pamoja haviliki.

Hivyo kwenye thamani nawapeni asilimia 25%

Nge na kaa Kushirikishana


Kwenye suala la kushirikishana mambo litawalindia sana issue ya nyie kuthaminiana kwa maana ndio kama nilivyosema hapo mwanzo kwamba thamani na kujali mahusiano yenu hajajui maana yake ndio maana linapokuja suala la kushirikishana utaona mmoja kati yenu anasema kuna muda ananithamini na kuna muda hanithamini hapana hayo ni matumizi mabovu ya maneno haya mawili na elimu ya kutofautisha hili hata muwe ni waelewa vipi kwenye hili la kuthaminiana hamuwezi kuendana wala kuelewana. 
Lakini kwenye issue ya kushirikishana na ushirikiano basi utaona kila mmoja wenu ni mwenye kujitoa kwa hali na mali katika kusaidia watu wanaomzunguka mwenza wake mfano yeye kujali ndugu zako na wewe kujali zake.
Yeye kutokana na hitaji lake la kimama kuwalinda watu anaewapenda, na wewe (Nge) ili kuweka mipaka mizuri juu ya kile uchofikiri ni sahihi. 
Ikiwa mtaunda dunia yenu ndogo yaani (nyumba yenu) basi utaona ni watu ambao ushirikiano wenu ni sawa na mapacha.

Hivyo kwa ushirikiano hapana shaka mnaendana kwa asilimia 95%

Summarize:

Mahusiano kati ya wawili nyie yanaweza kupiga kila siku hatua kutoka hatua moja kwenda nyingine. Kiukweli ni watu wenye kuendana sana na mahusiano yenu hushamiri kama umeoa au kuolewa na mtu haeleweki na umempata huyu basi muache yule kaa na huyu lakini kama upo nae kwenye mahusiano tu basi oa leo kabla ya kesho, na kama ni mtu una mfukuzia usikate tamaa.

NOTE:
Ikiwa unahitaji kutizamiwa nyota yako na mwenza wako ama mtu unaetaka kuhusiana nae na kujua mtaenda vipi, usisite kuwasiliana nasi:

Gharama sh elfu 15,000

Kwa mawasiliano na huduma:
Wasiliana nasi kupitia:

Email: rakimsspiritual@gmail.com
mnajimu@unajimu.com

WhatsApp +255 783 930 601

Rakims

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Check Now
Accept !