Nyota ya Mbuzi (Capricorn)

Rakims
0

 NYOTA YA MBUZI 

(CAPRICORN)

Hii ni nyota ya kumi katika mlolongo wa nyota 12. Nyota hii ni kwa watu waliozaliwa kati ya Tarehe 21 Disemba na 19 Januari au wenye majina yalio anza na herufi J au V au K.

Asili yao ni Udongo.Siku yao ya bahati ni Jumamosi. Namba yao ya bahati ni 8
Sayari yao ni Saturn (Zohal).

Malaika wake anaitwa Cassiel au Kafyaeel, na Jini anayetawala Jumamosi anaitwa, Abuu Nuhu au Aratron.

Rangi zao ni Nyeusi na Bluu iliyoiva. Wenye nyota hii wanashauriwa wapake rangi zifuatazo kwenye nyumba zao, rangi ya Kahawia (Brown) Rangi ya Kijivu (Grey) au Nyeusi (Black).

Rangi zinazowapa uwezo wa mapenzi, mahaba na furaha ya kujumuika na watu ni rangi za Hudhurungi (Puce) na Fedha (Silver).
Rangi inayowapa uwezo wa Kipato ni Rangi ya Samawi (Ultramarine).

Kito (Jiwe) ni Black Onyx. Madini yao ni Risasi (Lead).

Manukato yao ni yale yatokanayo na Msonobari (Pine), Maua yanayofanana na ya Jamii ya Choroko, Njegere au Dengu (Sweet pea) na Magnolia.


Nyota ya Mbuzi

MAMBO MUHIMU:-

Sifa ya Nyota hii ni Uongozi.

Ubora unaohitajika kusawazisha mambo ni kuwa wenye Uchangamfu na Furaha.

Maadili yao ni Uvumilivu, Utiifu, Ustaamilivu, Kuratibu, Kuandaa na Uwezo wa kuona mbali.
Matakwa yao ni Kutawala, Kusimamia na Kuongoza.
Tabia za kujiepusha nazo ni Kutokutegemea kuwa mambo mabaya yatatokea, Kuwa na masikitiko, Kutokupenda mabadiliko na Kupenda vitu na mali kupita kiasi.

USHIRIKIANE NA NANI?

Nyota za watu ambao anaelewana nao ni nyota za Ng’ombe na Mashuke.

Nyota za watu ambao haelewani nao ni nyota za Punda, Kaa na Mizani.

Nyota inayomsaidia kikazi ni nyota ya Mizani.

Nyota inayomsaidia kihisia ni nyota ya Punda.

Nyota inayomsaidia kipesa ni nyota ya Ndoo.

Nyota inayomsaidia katika ubunifu ni nyota ya Ng’ombe.

Nyota bora ya Mapenzi, Ndoa na Ushirikiano ni nyota ya Kaa.

Nyota bora ya kujifurahisha ni nyota ya Ng’ombe.

Nyota ambazo zinamsaidia katika mambo ya kidini na kiroho ni nyota za Mashuke na Mshale.

KIPAJI CHA MBUZI


Mbuzi wana kipaji cha kuchambua mambo kidogo kidogo au kufuatilia kitu bila watu kujua na kupata ufumbuzi wa uhakika mwishoni.Gradual

TABIA ZAO KIMAUMBILE NA KIMAPENZI


Mbuzi wanapenda kuwajibika, ni wenye bidii ya kazi, katika kazi yeyote watakayofanya hata kama ikiwa ni ya kipuuzi.
Ni viumbe waaminifu sana, watu wastahamilivu na wenye kuweza kuvumilia matatizo yeyote.

Kwa upande mwingine ni watu wenye tamaa kubwa ya kimaisha na kimaendeleo, na kwa sababu ya kutekeleza malengo yao basi huwa wanakuwa wabinafsi na wenye uroho na uchu.

Watu wenye nyota hii wanakuwa ni watu wenye aibu sana kwa wapenzi wao, lakini aibu ikishawaondoka huwa ni wapenzi wa kutisha, kwa maana ya kwamba kwa vile wao ni waaminifu wanataka wapenzi wao wawaunge mkono katika hisia zao za kimapenzi.

Ni watu wanaoogopa sana kuachwa na wapenzi wao hivyo basi huwa wanakuwa waangalifu sana katika kuchagua wapenzi.
Jambo jingine ni kuwa huwa wao wenyewe hawajiamini kimapenzi, mara nyingi wanashindwa kuingia katika mapenzi kwa woga tu hivyo kukosa nafasi nzuri ya kupendwa.

Kwa ujumla ni wapenzi makini na huwa hawaoi mpaka wapate uhakika wa kutosha kutoka kwa wapenzi wao. Ni wapenzi makini, waaminifu na wanaoweza kuaminiwa. Lengo lao katika mapenzi ni usalama.

KAZI NA BIASHARA ZA MBUZI

Mbuzi kitu muhimu katika maisha yake ni kazi na maisha mazuri na yanayoeleweka ambayo yako katika mpangilio wanaoutaka wao.
Ni watu ambao wanazingatia sana muda wa maisha na wana mpangilio maalum kwamba katika umri fulani awe amepata nini au awe na fedha kiasi gani.

Ni wenye kupenda utekelezaji wa kazi wa hali ya juu na wao wanapoagizwa hufanya hivyo.Kazi zao zinazowafaa ni zile za kutumia akili, Uhandisi, Usanifu Majengo, Saveya, kazi za Serikali, Siasa na Daktari wa Meno.

MAVAZI NA MITINDO

Mbuzi wanatakiwa wavae nguo za mitindo, zilizoshonwa kwa ustadi. Nguo hizo ziwe za rangi ya kijivu au Kijani iliyoiva au hudhurungi nzito.Kitambaa kiwe cha kitani (Linen) au cha ngozi.
Nguo ziwe ni suti na ziambatane na saa za mikononi.

MAGONJWA YA MBUZI

Nyota hii inatawala Mifupa, Magoti na Ngozi.Matatizo yao makubwa ya kiafya huwa yanasababishwa na muda mrefu ambao wanafanya kazi au kujishughulisha. Hii ni kwa sababu hawamwamini mtu mwingine afanye shughuli zao ambazo zina mipangilio ya muda mrefu,nguvu nyingi, na akili hutumika.

Shughuli zao nyingi za mizunguko na kufikiria huwaletea maradhi kama Baridi Yabisi (rheumatism).
Maradhi yao mengine makubwa ni ugonjwa wa Ngozi, matatizo ya Magoti na maradhi ya mifupa.

VYAKULA, NCHI, NA MIJI YA MBUZI

Mbuzi wanashauriwa wapende kula vyakula au matunda yafuatayo.ambayo ndio yanatawaliwa na nyota yao.Wapende sana vyakula vya Nazi na Nyama yeyote. Vile vile wapendelee kula Viazi Vitamu na Samaki Gamba (Shellfish).

Ili kupata mafanikio ya kinyota kwa watu wenye uwezo wanashauriwa aidha waishi au watembelee miji au nchi zifuatazo ambayo inatawaliwa na nyota ya Mbuzi.
Miji hiyo ni Brussels (Ubelgiji) na Oxford (Uingereza) au nchi za Mexico na India

MADINI, VITO NA MAFUSHO

Madini ya Mbuzi ni Risasi (Lead). Vito vyao vya kuvaa katika pete ni kama vilivyoonyeshwa katika picha hapa chini.
Mafusho ya Mbuzi ni Miatun- saila. unachoma siku ya Jumamosi kati ya saa 12-1 asubuhi na saa 7-8 mchana.



FUNGUO

Funguo ya mbuzi ni "natumia" basi yeye pale ambapo huwa anatumia vitu hovyo basi huzidi kupata vingine

Wasiliana nasi

Ikiwa ni mwenye kupendezewa na makala hizi, basi jihisi huru kuendelea kutufuatilia kupitia email lakini pia kama unahitaji mawasiliano yetu, tunapatikana kwa ajili ya misaada ya mfano wa makala hizi.

Unaweza kutupata kwa kupitia Email, vile vile kwa namba za simu, kupitia fomu ya mawasiliano katika tovuti yetu. Msaada wa kirafiki zaidi unatolewa na team yetu ya huduma kwa wateja na kujibu maswali yoyote ambayo unaweza kuwa nayo,

Ikiwa una maswali kuhusu makala zetu pia unaweza kuacha kwenye comment katika makala husika na kama ni huduma ya msaada wa tiba za kiroho au ushauri ama unahitaji kuagiza ama una suala lolote lingine basi tupo kwa ajili ya kutoa msaada pia.

Usisite kuwasiliana nasi kwa hekima za mawasiliano nifuraha yetu kusikia mahitaji ya wateja ama rafiki wa tovuti zetu za unajimu na RakimsSpiritual na tunatoa huduma nzuri za kumridhisha mwenye shida ikiwa tu atakidhi vigezo vya kuwa mteja ama rafiki wa tovuti hizi asante.

Na kwa maswali ya dharula kuhusiana na makala zetu kwa Members pekee;

Jihisi huru kututafuta masaa 24 ya week kupitia:-


Email: Rakimsspiritual@gmail.com au mnajimu@unajimu.com


WhatsApp: +255 783 930 601


Rakims

Tags

Chapisha Maoni

0Maoni

Chapisha Maoni (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Check Now
Accept !